Maranatha Media Kenya

Vitabu

Agape

Ndani ya kila mmoja wetu ni hamu ya Amani, utulivu na dhibitisho la kupendwa. Ni jinsi gani jamii ya mwanadamu inaweza ukaribia uhalisia huu? Na maendeleo haya yote katika teknolojia ulimwengu wetu yanaingia ndani zaidi katika ubinafsi na ukatili.

Maisha ya Kristo ambaye alitembea duniani miaka 2000 iliyopita yanatupa mfano wa upendo wa kujikana nafsi ambao umeleta amani kwa mamilioni yasiyohesabika. Kwa watu wengi upendo huu mzuri huangamizwa na hata kuharibiwa na hadithi nyingi ambazo zimenakiliwa katika kurasa za Bibilia zikielezea uhusiano wa Mungu na watu katika historia yote ya mwanadamu.

BABA NA MWANA - Makala ya Msingi

Sikuweza kutambua maana kamili ya kutambua kwamba Uungu wa Yesu ulipokelewa kupitia urithi Wake kwa Baba. Nikiibuka kutoka kwenye ukungu wa dhana ya uwongo kwamba uungu unaweza tu kuwa wa asili, na kwamba ukoo wake unaweza kuamuliwa tu na wakati unaoendelea milele, nilijikuta nikisimama katika msitu mnene wenye giza ambao ulitobolewa kwa ghafla na mwanga mkali. 

Kuelewa usawa wa Baba na Mwana katika suala la uhusiano lilikuwa wazo la kimapinduzi na zuri. Katika wazo hili moja, msingi mzima wa falme za kilimwengu ulivunjwa akilini mwangu. Nilisikia sauti ya kuugua, chuma kinachopinda na muundo wa mawazo niliyorithi ulianguka karibu nami na nuru ikaingia ndani ya roho yangu.

Hakuna maneno yanayoweza kuelezea hisia ya furaha niliyohisi.  Uzuri wa uhusiano wa Baba na Mwana uliniteka kabisa na nikapiga magoti mbele yao kwa mafuriko ya machozi. Katika wakati mmoja wa upweke nilikombolewa kutoka kwenye fumbo la Babeli na kuingia katika ufalme wa nuru. Hakika Mwana wa Mungu ndiye njia, kweli na uzima wa Baba.

Baba yetu Mpenda Rehema

Baba yetu Mpenda Rehema

Kama Uhukumuvyo

Kama Uhukumuvyo

Kujihatarisha Kwa Mungu

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu. upendo huo ulikuwa mkubwa sana Hata akahatarisha hazina yake aliyoipenda sana Mwana wake wa pekee ili kutuokoa

Kurudi Kwa Eliya

Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa. Luka 1:17

Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu. Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa; Na utukufu wa Bwana utafunuliwa, Na wote wenye mwili watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena haya. Isaya 40:3-5

Nitafunua vijito vya maji juu ya vilima, na chemchemi katikati ya mabonde; nitageuza jangwa kuwa ziwa la maji, na mahali pakavu kuwa vijito vya maji. Nitapanda katika jangwa mwerezi, mshita, mhadasi, na mbono; nitatia katika nyika mberoshi, mtidhari, na mteashuri pamoja; ili waone, na kujua, wakafikiri, na kufahamu pamoja, ya kuwa mkono wa Bwana ndio uliofanya jambo hilo. Mtakatifu wa Israeli ndiye aliyeliumba. Isaya 41:18-20

Ikumbukeni torati ya Musa, mtumishi wangu, niliyomwamuru huko Horebu kwa ajili ya Israeli wote, naam, amri na hukumu. Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya. Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana. Malaki 4 : 4-6

 

Mahubiri na Mazungumzo ya Mkutano Mkuu wa Minneapolis

“Iwapo tungekuwa na ufahamu wa haki ya umuhimu na ukuu wa kazi yetu na kujiona jinsi tulivyo wakati huu, tunapaswa kujawa na mshangao kwamba Mungu angeweza kututumia sisi tusiostahili kama tulivyo, katika kazi yake ya kuleta roho. Kuna mambo mengi ambayo tunapaswa kuelewa, ambayo hatuelewi kwa sababu tuko nyuma sana katika mapendeleo yetu.” [RH, Oktoba 8, 1889.2]

MASUALA YAHUSUYO MAISHA

Katika kitabu hiki Adrian Ebens anawasilisha njia ya baraka, ambayo inatiririka kutoka kwa Mungu kama chanzo cha uhai wote na ambayo inaweza tu kuhifadhiwa ikiwa kanuni mahususi na muhimu inatimizwa: utii. Uhusiano wa upendo kati ya Mungu na Mwanawe, ambao unajidhihirisha hasa katika kujisalimisha kwa hiari kwa Mwana kwa Baba, ni kanuni ya kimungu ambayo bila hiyo baraka hii haiwezi kuanzishwa.

Je, ungependa kujua jukumu lako ni lipi katika mkondo wa baraka na ni sehemu gani unayofaa? Je, unataka familia yako ipate baraka za Mungu kwa kiwango kubwa? Je, unataka kuwa na furaha?

Kitabu hiki kinafungua kutazama mtazamo wa juu zaidi wa muundo huu wa kiungu wa "mkondo wa baraka". Kwa msingi wa historia ya Biblia, inaonyesha umuhimu wa miundo ya familia iliyoimarishwa kimungu pamoja na matokeo ya jitihada za daima za Shetani za kuharibu njia hii ya baraka ili kuzuia baraka za Mungu ulimwenguni kwa ujumla na pia kwenye familia.

Katika kitabu hiki utapata majibu mengi, yakiwemo yale ambayo huenda bado maswali yake hayajaulizwa, kwa kuwa kanuni takatifu ya baraka bado haijatambuliwa kwa uwazi unaohitajika. Kwa hiyo, wale walio na njaa ya kiroho na wanataka kuzijua njia za Mungu vizuri zaidi, wanapendekezewa kusoma kitabu hiki kisicho na kifani. "Aha" uzoefu unaopatikana wa maisha ya furaha ni matokeo yasiyoepukika ya kitabu hiki.

Matendo ya Mungu Wetu Mpole

Matendo ya Mungu wetu mpole yanawasilisha ushahidi wa kutosha kuaminika kutoka kwenye Bibilia wa kumuondolea Mungu mashtaka kuwa yeye ni asiyejali, mwenye kuhukumu, mwenye kudhibiti, asiyehaki, mwenye hamaki, au katili. Kitabu kinadhihirisha kwamba Bibilia nzima, ikieleweka kwa usahihi, iko katika uiano na kifungu elezi: “Mungu ni Upendo” (1 Yohana 4:8)

Mfariji

Adamu alikabiliwa na chaguzi wakati mke wake alipomletea tunda lililokataliwa kwake. Alipochagua kukubali jaribio na kumfuata mkewe alimkataa Muumbaji wake. Je, nani sasa angekuwa chemichemi ya utulivu? Hawa alitolewa kwa Adamu ili awe msaidizi wake. Je, angeweza kumsaidia kukabiliana na mabadiliko yaliyotokana na kumuasi Mungu? Je, kuanguka dhambini kwa mwanadamu kulibadili vipi muungano huu? Je hili lilibadili vipi kipaji cha uzazi( tendo la ngono) kuhusiana na lile agano la zaeni mkajaze dunia?

Mmishonari kwa Ulimwengu - Matukio ya Joseph Wolff

Kabla ya 1844 kuja kwa 2 kwa Yesu kulihubiriwa ulimwenguni kote. Mtu mmoja, asiyeunganishwa na vuguvugu la Miller katika Marekani, alikuwa na ushawishi mkubwa zaidi katika kuhubiri ufahamu halisi wa kinabii wa Danieli na Ufunuo kuliko mwingine yeyote - Joseph Wolff - aliyejulikana wakati wake kama “Mmishonari kwa Ulimwengu,” moniker iliyokubaliwa na Ellen White, ambacho alikitumia katika kitabu chake Pambano Kuu.

Joseph Wolff alihubiri katika nchi ambazo hazijasikia injili ikihubiriwa kwa karne nyingi. Alizungumza na wafalme na wakulima, wavamizi wa watumwa na makahaba. Tuna mengi ya kujifunza kutoka kwake ikiwa tunataka kupeleka ujumbe wa mwisho wa rehema kwa ulimwengu unaokufa.

Mpendwa Wangu

Nasikia hatua zake, mapigo yangu ya moyo yanaenda kwa kasi kwa matarajio. Naisikia sauti yake kama mlio wa maji mengi. Ni kama zeri tamu nafsini mwangu. Mpendwa wangu anaita; inaweza kuwa ni kwa ajili yangu anaita? Ni vipi tumaini la thamani kama hilo linaweza kuzwa kifuani mwangu? Dhana hii inaibuka kutoka wapi? Mbona nihesabiwe kwamba nastahili utambuzi wake—Mfalme huyu mkuu, Mwana Mpendwa wa Baba? kwa huwahi ya patakatifu, Wimbo ulio bora na Mwendo wa Safari (Pilgrim’s Progress) tunaelezea safari ya mtu mmoja kupitia kwa vizingiti, majaribu na changamoto, kutambua, kuuza vyote na kuwa na upendo na Yesu, Mwana wa Baba.

Msalaba Uliotahiniwa na Msalaba Ulioshuhudiwa

Mbona msalaba ulihitajika na nani aliuhitaji?

Mbona msalaba ulikuwa muhimu kwa ukombozi wetu?

Je, ghadhabu ya Mungu iliridhishwa na kifo cha Mwanawe?

Haki ya Mungu ni nini na ina tofauti na haki yetu?

Mbona Yesu alijilinganisha na Nyoka wa shaba juu ya mti?

Patakati pa Waisraeli panatwambia nini kuhusiana na Msalaba?

Mungu ni Upendo!

Mzee Fifield anafunua upendo wa Baba 

mpole na asili ya kiroho ya sheria, upatanisho

 na mpango wa wokovu.

 

Dhana zinazoelezewa katika kitabu hiki hutoa mbegu 

ya msingi ya mawazo kwa ajili ya uelewa 

wa kweli wa tabia ya Mungu

Theos

Katika Kutafuta Mwana Mzaliwa wa Kwanza

Upatanisho

Ni hatua gani zinazohusika ili kupata upatano kamili na Mungu?

Je, Mungu anataka damu imwagike kabla ya kutusamehe? 

Je, Mungu alisababisha Mwanawe auliwe ili kulipa deni letu la dhambi? 

 Kwa nini Yesu alijilinganisha na kuinuliwa kama nyoka wa shaba? 

 Je, kuna umuhimu gani wa Musa kuupiga Mwamba pale alipoamriwa kuusemesha? 

Ikiwa wanadamu walichukuliwa mateka na Shetani, ni nani anayeweka bei ya fidia ili tuachiliwe?

 Je, Ubadilishaji wa Adhabu unahitajika kwa ajili ya Wokovu?

 Je, kifo cha Msalaba ni Upatanisho mbadala kwa ajili ya dhambi zetu? 

 Je, makanisa ya Kikristo yanafundisha ukweli kamili wa Upatanisho?

Utawala na Hatima

Katika miaka 200 iliyopita, uhusiano wa mwanadamu na vitu vya asili umebadilika sana baada ya kuendelea bila kubadilika kwa milenia. Mwanadamu amepata maendeleo ya ajabu, na maisha katika 2020 yamejaa miujiza ya kila siku ambayo ingeshangaza na kulemea watu wa vizazi vilivyotangulia.

Lakini juu ya maendeleo yote ni hisia kwamba hayawezi kudumu, kwamba yote yataanguka.  Ushahidi unaendelea kutokea ambao unaonekana kuashiria hofu zetu mbaya zaidi. Je! tulifikiaje hatua hii ya kipekee katika historia ya wanadamu? Je, wakati ujao unatuwekea nini? Je, kuna masomo kutoka kwenye maisha yetu ya zamani ambayo yanaweza kutupa ufahamu juu ya hali ngumu ya sasa? 

Waandishi wa kitabu hiki walikerwa na wasiwasi huu wa kudumu juu ya siku zijazo na kuhisi kwamba walikuwa wakikosa fumbo fulani la vipande ambavyo vilikuwa muhimu sana. Inaweza kuumiza kuchunguza mawazo yako mwenyewe na mifumo ya imani, lakini inaleta uponyaji ikiwa inafanywa kwa nia njema na upendo kwa wanadamu wenzako. Safari yao na ikutie moyo katika safari yako.

Vita vya Utambulisho

Vita vya utambulisho ni safari ya kujitambua binafsi. Ni makaribisho ya kujifunza kuhusu thamani yako katika muktadha wa mahusiano.

Maisha yetu yameshambuliwa na kelele ya ujumbe wa mara kwa mara ambao hutuambia kwamba mafanikio huja tu kutokana na kujidhibitishia wenyewe na kuthibitishia ulimwengu kuwa tuna kila kinachohitajika, kuwa tuna mambo sawa. Ni mfumo ambao hutufunza kuhisi kuwa na thamani na umuhimu wakati ambao tumefaulu na kufanikiwa kwa kiwango fulani. Matokeo ya mfumo huu yako na ushahidi kuwa sio mazuri. Mamilioni wako katika dhiki na mamia yanamaliza maisha yao katika kukata tamaa.

Nakukaribisha ujifunze hali ya kweli ya vita tulivyo ndani yake – vita vya utambulisho wa kile kinachofafanua thamani yetu na karama. Vigingi viko juu kwa kuwa ni uzima na mauti. Kitabu hiki kina safari yangu na kanuni nilizojifunza njiani. Uhuru ni kitu ambacho hutegemea lakini kitabu hiki kinaelezea barabara yangu kwa uhuru.