Maranatha Media Kenya
Mwandishi Adrian Ebens
Iliyochapishwa Apr 01, 2020
imeandikwa Apr 01, 2020
Vya kupakuliwa 877

Kuangamizwa kwa Sodoma na Gomora ni mojawapo ya hadithi muhimu za Bibilia zinazotumiwa na watu kuonyesha jinsi Mungu anaangamiza wale ambao hukataa kabisa kujisalimisha kwake. Moto ambao unatoka Mbingu unaeleweka kuwa Mungu mwenyewe anamimina ghadhabu ya moto kumaliza maisha ya wale wadhambi wasio na huruma ambao walikuwa mzigo kwao wenyewe na ushawishi mbaya ulimwenguni.

Lakini nini maana ya maneno ya Ufunuo kuhusu Sodoma?

Rev 11:8 Na maiti zao zitalala katika barabara ya mji mkubwa, ambao huitwa kiroho na Sodoma na Misri, ambayo pia Bwana wetu alisulubiwa.

Kristo alisulubiwa vipi huko Sodoma? Sio watu waovu wa Sodoma ambao waliharibiwa katika Sodoma? Inawezekana wengi wetu tumeangukia katika mtego wa kufikiria kuwa Kristo alipigwa na Mungu na kuteswa huko Sodoma wakati ni Kristo ambaye alisulubiwa kiroho hapo?

“Na wale pia waliomchoma.” Maneno haya hayatumiki tu kwa watu ambao walimchoma Kristo wakati alipokuwa akitundikwa kwenye msalaba wa Kalvari, lakini kwa wale ambao kwa kumtukana kwa uovu na kufanya vibaya wanampiga leo. Kila siku Anateseka machungu ya kusulubiwa. Kila siku wanaume na wanawake wanamchoma kwa kumdhalilisha, kwa kukataa kufanya mapenzi yake. {ST, Januari 28, 1903 par. 8}

Hadithi hii ni muhimu kwa sababu inaweka mfano wa kile kitakachotokea mwisho wa miaka 1000 kwa Sodomu waliopata kulipiza kisasi kwa moto wa milele. (Yuda 1:7)