Maranatha Media Kenya
Iliyochapishwa Sep 12, 2022
Vya kupakuliwa 175

Maneno ambayo Baba alizungumza na Mwanawe wakati wa ubatizo Wake yanatoa mwangwi wa baraka Aliyomimina juu Yake katika Sabato ya kwanza ya Uumbaji. Kila siku Baba alimfurahia Mwanawe, na Mwana alifurahi mbele zake. Siku ya Sabato Baba alimvuvia Mwanawe na Mwana aliburudishwa katika upendo wa Baba Yake. Uhusiano huu wa karibu kati ya Baba na Mwana uliwekwa kwa kudumu katika Sabato, na kila Sabato Baba hupulizia pumziko lake la kuburudisha juu ya Mwanawe na wale wote wanaomkubali Mwana.

Upendo wa Baba kwa Mwanawe ni wa kudumu, lakini unaonyeshwa kwa nyakati fulani zilizowekwa ambazo huakisi Kanuni ya Sabato. Tunapokuja kwenye miadi hii tunaingia katika furaha ya Baba katika Mwanawe. Tunapokuwa sehemu ya mwanamke anayesimama juu ya mwezi na kuvikwa jua (Ufunuo 12:2) tunajua nyakati na majira ya kuburudishwa kutoka kwenye kiti cha enzi cha Baba yetu.

Baba yetu sasa anatuita katika uzoefu kamili zaidi wa Sabato. Tumeitwa katika baraka zote za rohoni katika Kristo Yesu kama wana wa Ibrahimu (Wagalatia 3:27 29). Yesu anatuambia, “Tazama nasimama mlangoni nabisha” naye anabisha kwa wakati uliowekwa. Je! utamfungulia na kula pamoja Naye?